Psalms 65:1-6

Kusifu Na Kushukuru

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Daudi. Wimbo)


1 aEe Mungu, sifa zakungojea katika Sayuni;
kwako wewe nadhiri zetu zitatimizwa.

2 bEwe usikiaye maombi,
kwako wewe watu wote watakuja.

3 cTulipokuwa tumefunikwa kabisa na dhambi,
wewe ulisamehe makosa yetu.

4 dHeri wale uliowachagua
na kuwaleta karibu ili waishi katika nyua zako!
Tunashibishwa kwa mema ya nyumba yako,
mema ya Hekalu lako takatifu.


5 eUnatujibu kwa matendo ya kushangaza ya haki,
Ee Mungu Mwokozi wetu,
tumaini la miisho yote ya duniani
na la bahari zilizo mbali sana,

6 fuliyeumba milima kwa uwezo wako,
ukiwa umejivika nguvu,
Copyright information for SwhKC