Psalms 65:1-6
Kusifu Na Kushukuru
(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Daudi. Wimbo)
1 aEe Mungu, sifa zakungojea katika Sayuni;
kwako wewe nadhiri zetu zitatimizwa.
2 bEwe usikiaye maombi,
kwako wewe watu wote watakuja.
3 cTulipokuwa tumefunikwa kabisa na dhambi,
wewe ulisamehe makosa yetu.
4 dHeri wale uliowachagua
na kuwaleta karibu ili waishi katika nyua zako!
Tunashibishwa kwa mema ya nyumba yako,
mema ya Hekalu lako takatifu.
5 eUnatujibu kwa matendo ya kushangaza ya haki,
Ee Mungu Mwokozi wetu,
tumaini la miisho yote ya duniani
na la bahari zilizo mbali sana,
6 fuliyeumba milima kwa uwezo wako,
ukiwa umejivika nguvu,
Copyright information for
SwhKC